Jumatatu, 8 Julai 2013

MURRAY AWAFANYA WAINGEREZA KUGOMA KULALA KWA KURUDISHA HESHIMA YA WIMBLEDON TOKA 1936

Mchezaji namba 2 wa tenisi duniani Andy Murray amefaanikiwa kutwaa kombe la Wimbledoni na kuwa mwingireza wa kwanza kulitwaa kombe toka mwaka 1936 kwa mchezaji mmoja mmoja.

Murray alifanikiwa kuchukua kombe hilo baada kumfunga mchezaji namabri moja 1 Novac Dijokovic kwa seti  6-4 7-5 6-4 jumapili hii Uingereza.

Baada ya ushindi Waingereza walishindwa kuzuia hisia zao kwani miaka mingi pamoja na kuwa ndio waandaaji wa kombe hilo lakini walikuwa hawajawahi kulitwaa mpaka Murray alivyowarejeshea heshima.

Waziri mkuu wa Uingereza David Cameroon amesema Murray kainua morali ya nchi hiyo.
Akasema kuwa ilikuwa ni siku ya kubwa sana kwa mchezo wa tenisi uingereza na Uingereza kwa ujumla.

Mtendaji mkuu wa mchezo wa tenisi nchini Scotland  Daud Marshall ambako ndio asili ya Murray alisema kuwa anatumaini ushindi wa Murray utahamasisha vijana wengi kujiunga na klabu za tenisi za mtaani.

Marshall aliongezea kuwa klabu kubwa na mtani zote zimekuwa zikihakisha kuwa mchezo unakuwa karibu na vijana.
Kwa upande wa Waingereza wamegoma kulala na kushangilia ushindi huo huku wakiomba Murray ajengwe mnara wa heshima kwa kuipa heshima






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni